MAMA NA MWANA WAFA AJALINI IRINGA. WAZIKWA PAMOJA....
MIILI YA MAMA NA MTOTO IKIWA KWENYE MAJENEZA TAYARI KWA KUAGWA KATIKA HOSPITALI YA MKOA WA IRINGA BAADA YA AJALI
IRINGA
FRANK KIBIKI
MUUGUZI wa hospitali ya mkoa wa Iringa, Rose Stambuli
(56), na mwanae Daton Ilomo (23) ambaye ni mwanafunzi wa ICT katika chuo kikuu
cha mlimani, wamefariki dunia baada ya gari aina ya Noah walilokuwa wakisafiria
kupasuka taili, na kupinduka.
Ajali hiyo imetokea katika eneo la Igingilanyi, nje
kidogo ya manispaa ya Iringa na kuacha simanzi kubwa kwa ndugu jamaa na
marafiki, hususani mtoto pekee aliyebaki katika familia hiyo, Lusajo Mwakabuku.
Akisoma taarifa ya kifo hicho mara baada ya miili
hiyo, kuagwa hospitali ya Mkoa, Mmoja wa madaktari wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa
wa Iringa Dk Yahaya Msigwa amesema, mama alifariki juzi jioni wakati mtoto
akifariki leo.
Mama na mwanaye wote wamezikwa pamoja, katika makaburi
ya Makanyagio mjini Iringa baada ya kufanyika ibada katika kanisa la RC la
Mshindo.
Muuguzi huyo ambaye alikuwa na watoto wawili,
amemuacha mtoto mmoja Lusajo Mwakabuku ambaye ni mwanahabari kitaaluma.
Bwana ametoa na bwana ametwaa jina la Bwana
libarikiwe.
Amina
No comments:
Post a Comment