MATANGAZO

/zest+mkali+3.jpg /TULAMCHA+2+copy.jpg

Tuesday 30 July 2013

SITALIA TENA STORY YENYE KUSISIMUA, VISA NA MIKASA SOMA UJUE ZAIDI

STORY BARAKA R. LAZIMA
TITTLE SITALIA TENA
Danieli ni kijana aliekuwa msomi sana kakiri kutokana na ugumu wa maisha alijikuta kaingia kwenye matatizo makubwa sana, na kujikuta kapoteza dira ya maisha yake.  Hakujua la kufanya kujikuta akitoa machozi bila kikomo lakini alitafuta mbinu ya kujifuta machozi yaani alitoa kauli moja (sitalia tena je, alikuwa na maana gani basi fuatilia tamthilia hii ya kusikitisha sana na kusisimua sana sitalia tena.

Sehemu ya kwanza (1)
Daniel alikuwa kwenye gari la kifahari sana alikuwa mwenye mawazo sana lakini alikuwa na hamu sana ya kuona familia yake.  Akiwa anakaribia kufika nyumbani kwao alkuta mji apo kimya sana lakini alishangaa sana akiona mazingira yamebadilika sana, ulikuwa ni muda mrefu sana tangu aondoke nyumbani kwao.

Daniel akiwa anakaribia kufika nyumbani kwao alishangaa sana kuona anawaona watu wamejaa kwao, alishuka kwenye gari ili aone kunanini aliposhuka kwenye gari watu wengi walimwangalia kwa mshangao sana wengine walimuogopa sana lakini baadhi ya watu walimzuia asiingie ndani watu walio ndani walishangaa kusikia kelele walitoka nje, Daniel alishangaa sana kumwona binti mmoja ata yule binti alipomuona Daniel aliogopa sana na alimkumbatia mama yake huku akilia akisema katika tukio la siku ile ambalo tulitekwa na baadhi yetu waliuawa na wengine tulibakia basi mmoja wa watekaji huyu alikuwepo yaani (Daniel).  Machozi yalimtoka mama yake binti.  Jina lake aliitwa Doreen ni mke wa Daniel na yule binti ni mtoto wa Daniel lakini muda mrefu sana Daniel alikuwepo alimwacha mtoto wake akiwa mdogo sana miaka 5 na saizi ana miaka 12.  Daniel akiwa bado anamshangaa yule binti huku akikumbuka kitendo alichomfanyia, Doreen akaenda kwa hasira na kumzaba kibao Daniel, Daniel ni unyama gani umeufanya umefanya mabaya mangapi ukaona haitoshi na ukaenda kumwiba binti yako, Daniel alishangaa sana kusikia kauli hiyo, Daniel akamuuliza Doreen anasema huyu binti ni mtoto wangu, Doreen akajibu ndio ni damu yako, Daniel akajikuta akitoa machozi na kuomba msamaha akidai hana maisha tena, kwa unyama aliufanya akaomba msamaha lakini yule binti alilia sana na akasema wewe sio baba yangu mimi sina baba, Daniel yale maneno yalimuuma sana yakamfanya alie kwa uchungu huku watu wakimshangaa.  Pia Daniel alimwomba mke wake amuitie mama yake amuombe msamaha, Doreen akamshangaa Daniel akamwambia kweli wewe ni shetani ulie changanyikiwa ulifikiri umekuja baada ya kusikia mama yako kafariki huoni umati wa hawa watu, Daniel hakuamini machoni mwake kuambiwa maneno hayo, moyo wake ulimuuma sana na kujikuta anabubujikwa na machozi alikuwa na maumivu makali moyoni mwake.  Daniel alimpenda sana mama yake alienda kutafuta maisha kwa ajili ya familia yake hakuamini machoni mwake akiwa na mawazo kichwani mwake akaingia kwenye gari akaendesha kwa kasi huku akinywa pombe kali kwa hasira yote hayo alowatamu mtu mmoja.  Alikuwa mwendo kasi akielekea kumuongamiza mtu huyo.  Lakini mawazo yake akaona bora aende kituo kikuu cha polisi ili aonane na kamanda wa polisi kwani alimuamini sana mtu huyo kwani Daniel alizijua sana siri nyingi za nchi.

Daniel akiwa anaelekea kituo cha polisi lakini alijua kuwa anatafutwa kwa muda mrefu na polisi, akapata jibu jinsi ya kuingia kituo cha polisi.  Daniel alikuwa na silaha kali kali sana liingia duka moja jirani na kuwataka baadhi ya watu na kuwaagiza kwenye gari na kuwahinga pingu alikuwa na silaha nyingi sana aliendesha gari kwa kasi sana wale matekwa walishangaa kumuona mtekaji anaelekea kituo kikuu cha polisi, Daniel alipofika karibu na kituo cha polisi alishangaa polisi wakiwa bize na magari yao huku wakiwasha king’ora basi yao alipishana nao.  Kumbe polisi walipigiwa simu kuhusu watu waliotekwa lakini polisi hawakutambua lile gari kwani hawakupewa taarifa kwa undani magari mengi yalimpita Daniel.  Kituo cha polisi kilibakia na askari wachache sana.  Daniel alishuka kituo cha polisi huku akiwashirlia wale mateka na akiwa ameshika mabomu mkononi na mashine kubwa sana ambayo baadhi hata askari hawajawahi kuona atakusikia bunduki ile ombi la Daniel lilikuwa moja akiwambia askari  waliojificha ndani ya kituo cha polisi huku wengine wakiwapigia simu akdari walioenda kumtafuta mtekaji.  Daniela aksema sina ubaya na jeshi la polisi naomba nionane na kamanda wenu ndani ya dakika 5 msipofanya hivyo wale mateka atakuwa halali yangu pamoja na hiki kituo chenu.  Askari walikuwa hawajibu wakamuomba mkuu wao aikilize maelezo ya Daniel, mkuu wa kamanda alikuwa mbali kutokana na uzalendo wake na kuapa alichokula akuogopa kituo maisha yake kwa ajili ya raia wake aliopewa dhamana na kuwalinda kwa mujibu wa katiba ya muungano wa Tanzania,  akatoka nje na akiwa ameweka mikono juu na huku akijitambulisha kuwa yeye nide kamanda wa polisi. Daniel alicheka kidogo kasha akatoa machozi akisema wewe tangulika mbali sana ongera kwa kazi nzuri sana.

Kamanda wa polisi alishangaa sana kusikia yule mtekaji anamjua vizuri, Daniel akajitambulisha jina lake pia akamuomba kamanda najua unalijua sana jina hili ni mimi mwenyewe ulikuwa unanitafuta kwa muda mrefu sana kamanda hakuamini machoni mwake na pia alishangaa sana.  Na kumuuliza Daniel naomba uwaachie hao watu.  Daniel akajibu sina shida na hawa watu naomba tuongee na wewe mimi si muhalifu tena nimekuja na mambo mengi sana tafadhali niamini kamanda alimsikiliza kwa makini Daniel kasha akamsogelea Daniel alikuwa na pingu mkononi akamshika kamanda akajifunga nae huku akisema kwenye kiuno changu nimevaa mkanda wa bomu endapo vijana wako watafanya lolote nitaacha fyuzi bomu litalipuka tutakufa wote, kamanda akatoa amri kwa vijana wake wasifanye lolote.  Daniel akamwambia kamanda kuwa nina siri kubwa sana ila kabla ya yote naomba tuende nyumbani mkamzike mama yangu baada ya hapo nitakuambia kila kitu.  Kamanda akatoa amri baadhi ya vijana wake waongozane.  Daniel aliomba watumie gari lake na pia katoa amri kuwa wote mateka waachiwe hana ugomvi nao bali ilikuwa ni njia kuu ya kufika hapo kituo cha polisi.  Daniel akawaomba radhi na kusema poleni sana msiogopoe sina nina ya kuwazuru mmenisaidia tu lengo langu la kuwateka nilitaka kuonana na huyu mheshimiwa.  Daniel akamfungua mlango wa gari na kuwaamuru askari mmoja achukue kitita cha fedha awapatie wale mateka kama kuwapotezea muda wale mateka hawakuamini kupewa fedha nyingi kiasi kile. Daniel akiwa kajifunga pingu na kamanda wa polisi wakaingia kwenye gari na kuelekea kwenye msiba wa mama yake huku askari akiwa anendesha gari.  Walipofika nyumbani alimkuta watu wanafanyika kutoka makaburini.  Daniel aliumia sana.

Umati wa watu walishangaa sana kuona magari ya polisi na kumuona kamanda wa polisi akiwa amejifunga pingu na Daniel.  Daniel aliwafuata mke wake na kuomba akamuonesha alipopumzika mama yake.  Daniel akamfungua pingu kamanda na akajifunga yeye na akamkabidhi huyu kamanda na akamwambia kuwa yeye sio muhalifu tena amuamini maneno yake.  Daniel akiwa chini ya ulinzi wakampeleka makaburini.  Daniel alioneshwa alipolala mama yake.  Daniel alilia kwa uchungu sana na kumuahidi mama yake kuwa anatugokoa lakini sio muda atamfuata yeye kuomba msamaha. Doreen aliongea kwa uchungu huku akimwambia Daniel kilio cha mama yako kimesababishwa na wewe.  Mama yako alipata ugonjwa kiarusi baada ya kusikia unatafutwa na polisi huku vyombo mbalimbali vya habari vikiandika jina lako unatafutwa, maneno yale yalimuuma sana Daniel akamwambia mke wake achukue begi ndani ya gari lilikuwa na pesa nyingi sana, kasha Daniel akmwambia mke wake leo itakuwa ndo mwisho wa kunana kwani aendako ajui kama atakuwa salama alimkabidhi na hati mbalimbali za mali zake na kumweleza mahali zilipo kasha Daniel akamuomba mkuu wa polisi ampeleke kituo cha polisi akamweleze kila kitu na kumwambia anazo siri nyingi sana.

Daniel akamuaga mke wake huku akitokwa na machozi wote kwa pamoja walilia sana.  Daniel akiwa chumba maalum cha polisi akiwa na wakuu wa kituo. Kamanda akamuuliza Daniel tueleze kwanini ulifanya matukio makubwa namna hii na kiongozi wako ni nani alikuwa anakutuma?  Daniel aliinama kichwa chini huku akitokwa machozi kasha kaaza kusimulia mkasa wote tangu utotoni mwake.  Fuatilia kisa hiki ujue hatima ya Daniel.

3 comments: