MATANGAZO

/zest+mkali+3.jpg /TULAMCHA+2+copy.jpg

Tuesday 11 March 2014

HATIMAYE AJIRA MPYA ZA WALIMU KUTANGAZWA TAREHE 15, TAARIFA TOKA TAMISEMI HII HAPA

Written By Kitaani Bongo on Tuesday, 11 March 2014 | 03:25


OFISI ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imetangaza ajira mpya za walimu wapya 36,021 waliohitimu mafunzo ya uwalimu mwaka 2013.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa TAMISEMI, Jumanne Sagini alisema walimu hao wataajiriwa na mamlaka za Serikali za Mitaa, Aprili mosi mwaka huu.
Alisema kati ya idadi hiyo, walimu wa ngazi ya cheti (Daraja III A) ambao watafundisha shule za msingi ni 17,928 na walimu wa shule za sekondari 18,093 wakiwemo 5,416 wa stashahada na 12,677 wenye shahada.
“Orodha rasmi ya walimu wapya ambayo itaonesha halmashauri mbalimbali walizopangiwa walimu hao itatangazwa kwenye tovuti ya TAMISEMI na ile ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Machi 15 mwaka huu,” alisema Sagini.
Aliongeza kuwa, walimu hao wanatakiwa kuripoti kwenye halmashauri husika walizopangiwa ifikapo Aprili mosi mwaka huu ili taarifa zao za kiutumishi zifanyiwe kazi na waajiri wao ambao ni Wakurugenzi ili waweze kupata mishahara yao.
“Upangaji walimu wapya kwenye halmashauri umezingatia uwepo wa mahitaji ya walimu, fedha za kujikimu kwa muda wa siku saba na nauli ambazo zitalipwa kwa kila mwalimu ambaye ataripoti kulingana na viwango vilivyowekwa na Serikali,” alisema.
Aliongeza kuwa, TAMISEMI haitafanya mabadiliko yoyote ya vituo vya kazi kwa walimu wapya isipokuwa kwa utaratibu wa kawaida wa uhamisho

credit by tamisemi website, habari hii ni ya kweli wala si uzushi waweza kwenda kwenye website ya  tamisemi kwa kubofya link hii hapa   www.pmoralg.go.tz ,
bofya hapa kuona

No comments:

Post a Comment