Sababu za kupotea kwake;
Ukiongelea jina kama Z-anton kwa wengi watakuwa wanamjua msanii huyu maarufu kwa wimbo wake uitwao binti kiziwi,unaweza
kusema kuwa ni moja ya waasisi wa muziki huu wa bongo fleva, ambao
wameweza kukusanya wapenzi wengi wa muziki huu wa bongo fleva,nakuweka
mchango mkubwa katika kukuza muziki huu na kufanya uweze kupendwa na
mashabiki wa kila rika…na kama ulikuwa unajiuliza huyu mtu yuko wapi,..
he is back! anakuja tena na nguvu mpya hivi sasa katika game hili la
muziki wa bongo fleva.
Akiwa anahojiwa na kipindi kimoja cha
television nchini Kenya amefunguka nakusema kuwa upotevu wake katika
game la muziki huu,ni kutokana na matatizo ya hapa na pale yakifamilia
na kibinafsi zaidi aliyokuwa anakabiliana nayo,ila kwa hivi sasa its all
gud,yuko teyari kurudi kwenye game.
Kuhusu muziki wake;
Kuhusu muziki anafunguka na kusema kwa
sasa amerudi katika game na nguvu mpya kabisa,ingawa kulikuwa na baadhi
ya watu waliokuwa wanamwekea vizingiti ili asiweze kurudi katika game
hili la bongo fleva,ila kwa hivi sasa anarudi kipekee zaidi,hii yote ni
baada ya kujitoa katika kundi lake la zamani la tiptop connection na
kuongezea kuwa hana mpango hata wakurudi kundini cause anataka kufanya
masuala yake ya muziki mwenyewe,bila ya kutegemea mkono wa mtu yeyote
Yule kwa hivi sasa.
Maisha yake ya mahusiano baada ya binti kiziwi kukamatwa;
Rumors zilikuwa za kweli kwamba mpenzi
wake aliyekuwa amekamatwa huko nchini china amefungwa kutokana na kosa
la kuingiza madawa ya kulevya,na zaidi ni kuwa huko aliko anatumikia
kifungo cha miaka sita,ila kwa upande wa Z-anton, hayo yote hayamhusu
kwa sasa ,cause walishatemana siku nyingi na habari ya mujini ni kwamba
hivi sasa anampenzi mwingine ambaye wamefanikiwa kupata mtoto mmoja.
No comments:
Post a Comment