Mwili wa marehemu Mussa ukiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga wakati wa kufanyiwa postmoterm leo |
Mwili wa marehemu Mussa ukiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga wakati wa kufanyiwa postmoterm leo |
Wakazi wa shinyanga wakijiachia kwenye tamasha hilo masaa machache kabla ya tukio. |
Tamasha maarufu nchini hapa linaloratibiwa na
kikundi cha Clouds media Group, chini ya udhamini wa kinywaji cha Serengeti
maarufu kama “SERENGETI FIESTA” na mwaka huu Tamsha hilo
likiwa na kauli mbiu yake iitwayo “SAMBAZA UPENDO” limeingia dosari baada ya kutokea
mauaji wakati tamasha hilo
likiendelea.
Kijana
mmoja aliyejulikana kwa jina la Mussa Shija (17) mkazi wa kata ya Chibe katika manispaa ya
Shinyanga aliyeuawa kwa kupigwa kitu kizito kichwani na watu wasiofahamika
akiwa kwenye tamasha la Serengeti Fiesta lililokuwa linafanyika usiku wa
kuamkia leo katika uwanja mdogo wa Kambarage mjini Shinyanga
Akizungumza na Malunde1
blog mganga mfawidhi wa hospitali ya mkoa wa Shinyanga Dkt Fredrick Mlekwa
amesema uchunguzi wa kitaalam walioufanya unaonesha kuwa kijana huyo
alipigwa na kitu butu kichwani na kusababisha kuvuja damu kichwani kutokana na
kuvunjika kwa fuvu la kichwa.
Kaimu kamanda wa polisi
mkoa wa Shinyanga Mussa Athuman amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na
kuongeza kuwa uchunguzi wa awali unaonesha kuwa kijana huyo aliuawa kwa
kushambuliwa na watu wasiojulikana nje ya fensi la uwanja mdogo wa Kambarage
palipokuwa panafanyika tamasha la Fiesta.
Hata hivyo amesema jeshi
la polisi litatoa taarifa kamili baadaye kwani linaendelea kufanya uchunguzi
No comments:
Post a Comment