MATANGAZO

/zest+mkali+3.jpg /TULAMCHA+2+copy.jpg

Wednesday, 3 July 2013

CHELSEA NA ARSENAL WAMGOMBANIA STRAIKA ROONEY

Wayne Rooney

Nyota wa Manchester United Wayne Rooney asherehekea baada ya kufunga bao mechi ya awali. Picha/AFP 

Na MASHIRIKA
Imepakiwa - Wednesday, July 3   2013 at  07:49
Kwa Mukhtasari
Arsenal na Chelsea zinatega masikio kwa makini kusikia yanayoendelea kuhusu straika wa Manchester United, Wayne Rooney baada ya kubainika kuwa mwanasoka huyo atahama klabu.

LONDON, Uingereza
ARSENAL na Chelsea zinatega masikio kwa makini kusikia yanayoendelea kuhusu straika wa ManchesterUnited, Wayne Rooney baada ya kubainika kuwa mwanasoka huyo atahama klabu Rooney alitarajiwa kukutana na kocha wake, David Moyes kutatua shida yake ya kuchoshwa na klabu lakini kulingana na vyombo vya habari nchini Uingereza, wawili hao walikutana mwezi jana na ilidaiwa kuwa hawakuafikiana.
Katika mazungumzo ya wiki hii, Rooney anatarajiwa kufanya uamuzi wake akisaidiwa na ajenti wake, Paul Stretford na mwenyekiti mpya wa Red Devils, Ed Woodward.
Moyes hajakata tamaa kumshawishi Rooney kuipatia Man United nafasi nyingine lakini kinachosubiriwa sana ni majibu kuhusu ni lini atakapoondoka mwanasoka huyu, na ni klabu ipi atakayohamia.
Maajenti wake wanatarajiwa kusisitiza kuwa mwanasoka huyo anataka kuhama klabu kufuatia msimu uliopita.
Rooney alipuuzwa na aliyekuwa kocha, Alex Ferguson kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Real Madrid na kushuku ukakamavu wake.
Mwanasoka huyo pia alichezeshwa katika safu ya kati, kufuatia kuwasili kwa Robin van Persie ambaye sasa amekuwa chaguo la kwanza la mashambulizi.
United inajiandaa kwa mechi za kirafiki katika ziara za Mashariki ya Mbali na Australia juma lijalo na mechi hizi huenda zikawa za mwisho kwa straika huyo mwenye umri wa miaka 27.
PSG
Rooney ananyemelewa na mahasimu wa United, Arsenal na Chelsea huku Real Madrid na Paris Saint-Germain zikiwa macho. Iwapo ataamua kuhama, huenda Moyes akamwuza kwa klabu nje ya Uingereza, kwani kupeana nyota huyo kwa Chelsea au Arsenal, itakuwa sawa na kumpa silaha adui.
Kiungo stadi wa Arsenal, Jack Wilshere ambaye ni Muingereza mwenza wa Rooney amesema klabu yake itaimarika pakubwa ikifaulu kumnunua.
“Iwapo itawezekana, basi itakuwa hatua ya kuvutia sana. Rooney ni aina ya mwanasoka ambaye anaweza kufanya chochote hadi mkashinda taji la Ligi Kuu. Kumwona katika orodha ya kikosi cha kwanza kunawatia wasiwasi mahasimu na tunaweza kushinda mataji mengi sana akiwasili,” Wilshere alisema.

No comments:

Post a Comment