"aaa ukweli ni kwamba sijui anachokitengeneza yeye, mimi ndio nimefunga
show mbagala, hakuna kitu kama hicho kilichotokea,unajua mi nilikua
nimerusha flana niliyokuwa nimevaa, watu walikuwa hataki niimbe nikiwa
na flana, so baada ya kuirusha ile flana ndio watu wakaanza kusukumana
huku na kule, umati ulikuwa mkubwa, aah ikabidi wakadondokea ile mashine
ambayo ilikua inapiga mziki pale, nafkiri show ndio ikaishia pale.na
nimeondoka pale nikisindikizwa na umati wa watu mia mbili au mia tatu,
mi nilikua kwenye boda boda wamenisindika mpaka ndani Dar Live.
Chidi amendika kitu kama hicho so sijui anataka kunitengenezea CV gani,
lakini hakuna kitu kama hicho kwanini, mimi ndio nimefunga show,
walikuwa wanasubiri show yangu mimi, kila mtu alikua anataka kuongea na
mimi hata kunigusa tu, kila mtu alikua anataka kuongea na mimi, hata
kunigusa tu...."
Chidi ajipange amechezea bahati alipata line nzuri kafanya mambo ya
ajabu, mwisho wa siku amepotea, anahisi na mimi naweza nikapotea kama
yeye, mi najua nafanya nini, mi mtoto wa kihuni ambae nimetokea mbali,
nimepitia mengi, sijatengenezwa kama yeye alivyotengenezwa, nimefight
mpaka leo mashabiki wananielewa.
Hiki ndicho alichokuwa amekiandika Chidi kwenye ukurasa wake wa facebook

No comments:
Post a Comment