MATANGAZO

/zest+mkali+3.jpg /TULAMCHA+2+copy.jpg

Sunday, 7 April 2013

HUU NI UJIO MPYA WA MSANII ZAX B KUTOKA MBEYA NYIMBO MAMA NISAFIRISHE

Msanii Zax B anayefanya vizuri sana pande za nyanda za juu kusini katika anga ya muziki wa bongo flava maskani yake yakiwa jijini Mbeya akiwakilisha kundi la Homestigers ambao wanafanya vizuri mbeya anawaomba mashabiki wake wampokee vizuri kwa ujio mpya wa ngoma yake kali inayoitwa Mama nisafirishe baada ya kimya cha muda mrefu.Baada ya kuhojiana naye pande za Mbeya mjini na hicho ndicho alichosema."yap mziki nimeanza zamani lakini ndo hivyo kama unavyoisikia nyimbo hii kiukweli iko vizuli na hii ni baada ya ile nyimbo yangu ya mwisho iliyofanya vizuri pia iliotambulika kwa jina la napenda muziki, na kikubwa ni support kutoka kwa mashabiki ambao wanafeel mziki wangu na naamini mambo yatakuwa vizuri tuu kwani nakalibia kumaliza video ya nyimbo hii ili kukamilisha album yangu itayofahamika kwa jina la mama nisafilishe".Alisema Zax B

No comments:

Post a Comment