MATANGAZO

/zest+mkali+3.jpg /TULAMCHA+2+copy.jpg

Wednesday, 17 April 2013

FIFA WAKUTANA NA WIZARA YA VIJANA,UTAMADUNI NA MICHEZO


                                          Taarifa Kwa Vyombo vya Habari

Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo leo tarehe 17 April, 2013 imekutana na ujumbe wa FIFA ulioongozwa na Bw. Primo Corvaro ambao umekuja Wizarani kwa ajili ya kujitaMbulisha. Ujumbe huo umekutana na Katibu Mkuu, Bw. sethi Kamuhanda kwa niaba ya Waziri Mhe. Dkt. Fenella Mukangara ambaye yuko safarini.

Katika utambulisho huo, ujumbe wa FIFA umemweleza Katibu Mkuu kwamba wamekuja kufanya tathmini ya matukio yaliyojitokeza wakati mchakato wa uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF).

Wameeleza kwamba tathmini yao itajikita katika Kukusanya taarifa mbambali kutoka kwa makundi mbalimbali yakiwemo ya wagombea walioenguliwa na kisha kuwasilisha maoni na uchambuzi wao Makao Makuu ya FIFA mjini Zurich, Uswisi kwa majadiliano zaidi na baadaye kutoa ushauri wa namna ya kumaliza changamoto iliyopo.

Aidha, ujumbe huo umeeleza kwamba walilazimika kuja nchini Tanzania baada ya ya kupata malalamiko kutoka kwa wagombea walioenguliwa katika kinyang'anyiro cha uongozi na baadaye kuombwa na TFF kuja kuwasikiliza walalamikaji.

Akipokea salaam zao, Katibu Mkuu kwa niaba ya Waziri aliushukuru ujumbe huo kwa ujio wao ambao alsema anaamini utaweka mazingira rafiki ili uchaguzi ufanyike bila malalako tena. Aidha ailishukuru FIFA kwa mchango mkubwa inaotoa kwa ajili ya maendeleo ya mpira wa miguu nchini.

Aliwahakikishia wajumbe hao kwamba serikali yetu itaendelea kushirikian na FIFA kwa ari na mali ili kuhakikisha mpira unasonga mbele kwa amani na utulivu.

No comments:

Post a Comment