MATANGAZO

/zest+mkali+3.jpg /TULAMCHA+2+copy.jpg

Friday, 19 April 2013

UBINAFSI WA REAL MADIRD NA BARCELONA WAVIFANYA VILABU VINGINE VYA LA LIGA KUDAIWA KODI NA SERIKALI ZAIDI YA $870 MILLION


Malaga moja ya timu zinazoongoza kwa madeni na zipo kwenye hatari ya kufilisika
Vilabu vya soka vya Spain vinadaiwa kodi na serikali ya nchi hiyo inayokadiriwa kufikia 670 million euros ($874 million), limesema baraza la michezo la nchi hiyo juzi Alhamisi.  

Rais wa baraza hilo Miguel Cardenal alisema kiasi cha kodi ambacho vilabu vinadaiwa na serikali kimeshuka kutoka 750 million euros ($979 million).
Cardenal aliiambia radio taifa ya Spain kwamba kupungua kwa deni hilo ni jambo zuri lakini vilabu vinabidi vitafute namna nzuri ya kugawana mapato ya haki za matangazo ya TV ili vijihakikishie kuepukana na shida za kiuchumi. 

UEFA wameifungia Malaga kushiriki mashindano ya ulaya kwa msimu mmoja kwa kushindwa kulipa mishahara ya wachezaji na kulipa kodi kwa muda - adhabu hiyo ikiwa moja ya njia ya kuilazimisha klabu hiyo kutimiza wajibu wake. 
 
Cardenal alisema kwamba wanataarisha sheria ya kuvilazimisha vilabu kuuza haki za matangazo za mechi kwa umoja, badala ya umimi uliopo kwenye biashara hiyo hivi sasa.

No comments:

Post a Comment