MATANGAZO

/zest+mkali+3.jpg /TULAMCHA+2+copy.jpg

Sunday, 21 April 2013

MARCO CHALI ASEMA WASANII WAKIZINGATIA HAYA WATAFANIKIWA


mako
Producer Marco Chali kutoka MJ Records. Picha na Mwananchi.
Licha ya kuongezeka kwa studio za uzalishaji wa muziki kona  za vichochoro vingi vya Jiji la Dar es Salaam, yeye ni mmoja kati ya wazalishaji wachache  wenye uwezo na kujiamini kwa kuzalisha muziki wa kizazi kipya maarufu kama Bongo fleva hapa nchini.
Huyu ni Marco Marthias maarufu kama Mako Chali, mwenyeji wa Mji wa miamba(Mwanza), aliyeingia studio za MJ Rekod miaka ya 2006. Katika hesabu za haraka mwenyewe anathibitisha kuandaa zaidi ya kazi 4000 za wasanii mbalimbali tangu alipoingia studio hizo. Mako  aliye katika studio hizo zilizopo Masaki jijini Dar es Salaam,anapata nafasi ya kuzungumzia ubora wa msanii, changamoto, udhaifu na kazi wanazozifanya.
Anasema kuwa thamani ya msanii wa bongo na maslahi wanayoyapata ni vitu viwili tofauti. “Msanii wetu anayefanya vizuri katika muziki huu anatakiwa kulipwa maslahi yanayoendana na thamani yake, kiwango cha chini kwa wasanii waliopo katika soko kwa sasa wanatakiwa kupata kati ya Sh18 na 20 milioni kwa shoo moja,”anasema Mako.

No comments:

Post a Comment