Monday, April 15, 2013
Katibu Mkuu wa timu hiyo, Salum Kaguna amesema jijini Dar es Salaam kuwa wameliandikia barau TFF kutaka mechi hizo zisogezwa.
"Tunafikiri iwapo tutamaliza ligi kabla ya timu nyingine, wanaweza kutumia mwanya huo kupanga matokeo."
"Kwa hiyo, tunaitaka TFF kuhakikisha mechi zetu mbili zinasogezwa mbele ili kuleta usawa wa timu zote kumaliza ligi kwa pamoja." alisema Kaguna.
Alisema iwapo timu hiyo itamaliza mechi zake mapema, timu za African Lyon, Polisi Moro na JKT Ruvu ambazo zipo kwenye hati hati ya kushuka daraja sawa na Toto African zinaweza kutumia nafasi hiyo kupanga matokeo kujinusuru na mkasi huo.
Kwa mujibu wa ratiba ya ligi ya TFF inaonyesha kuwa Toto African itacheza mechi yake kesho dhidi ya Kagera Sugar kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza na kumalizia na Ruvu Shooting ya Pwani.

No comments:
Post a Comment