MATANGAZO

/zest+mkali+3.jpg /TULAMCHA+2+copy.jpg

Thursday 10 October 2013

MAN UNITED HUENDA IKAWAPOTEZA WACHEZAJI WAKE WANAOKOSA NAMBA KIKOSI CHA KWANZA

 
Fabio Da Silva anataka kuondoka Manchester United baada ya kusema ameshindwa vita kupata namba katika kikosi cha kwanza ndano ya Old Trafford.

Ingawa kaka yake Rafael amekuwa katika kikosi cha kwanza cha United katika nafasi ya ulinzi wa kulia Fabio anakuwa nyuma ya walinzi wengine wa kushoto Patrice Evra na Alex Buttner .
Pengine lingekuwa ni anguko kubwa kabisa kwake endapo David Moyes angefanikiwa kuwanasa Leighton Baines au nyota wa Real Madrid Fabio Coentrao wakati wa uhamisho wa majira ya kiangazi
Fabio mwenye umri wa miaka 23 alitumia msimu uliopita kwa mkopo katika klabu ya QPR na ameitumikia United mchezo mmoja katika kampeni ya mwaka huu.
Alikuwa ni miongoni mwa  wachezaji watatu wa kikosi cha kwanza wakiwemo akina Ashley Young na Buttner, katika mchezo wa kirafiki uliochezwa bila ya watazamaji dhidi ya Barnsley siku ya Jumatatu.
Fabio, ambaye aliwasili pamoja na ndugu yake Old Trafford wakitokea katika klabu ya Fluminense mwaka 2008, amemuambia Moyes kuwa anapendea kuondoka mwezi Januari na angependelea kurejea nchini Brazil.

No comments:

Post a Comment